Promote your business for free

THIS BLOG IS SPONSORED BY AFRICAN SOCIAL NETWORK ,THE SOCIALY NETWORK PAY ITS USER IN POINTS BASED JOIN NOW AND SEE HOW MUCH MONEY YOU CAN MAKE USING SOCIAL NETWORK. | FEEL FREE TO ADVERTISE ON WWW.BONGLOB.COM

Monday, 19 July 2010

JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA



WIZARA YA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI


UTANGULIZI


Kuna umuhimu mkubwa sana kwa kila Mtanzania kujua maana ya soko la

pamoja la Arrika Mashariki na taratibu zinazolizunguka soko hilo.

Kutokujua jambo hili ni hatua na dalili za awali za kushindwa

kukabiliana na changamoto zitazotokana na soko hili.Hii ni kweli

kwakuwa kama Mtanzania hajui nini maana ya soko la pamoja,ni maeneo

gani soko la pamoja au ushirikiano huu unahusika nayo na nini

kinafanyika na kwa vipi, bila shaka Mtanzania huyu hawezi pia

kushindana ma wenzake kutoka nchi washirika katika soko hili.

Kipeperushi hiki kimeandaliwa ili kumwezesha Mtanzania hasa Mtanzania

wa kawaida kuweza kujua hata kwa kiwango cha chini mambo ya msingi

yanayolizunguka soko hili ili iwe hatua ya awali kwake katika

kukabiliana na changamoto kutoka nchi washirika.


1. NINI MAANA YA SOKO LA PAMOJA LA AFRIKA MASHARIKI

Maana ya soko la pamoja la Afrika Mashariki , ni kiwango cha juu cha

ushirikano wa kiuchumi baina ya nchi washirika ambao unahusisha maeneo

nuhimu kama, uhuru wa kubadilishana bidhaa, uhuru wa kubadilishana

huduma,uhuru wa kubadilishana wafanyakazi, uhuru wa kubadilishana

mitaji na uhuru wa kuanzisha makazi popote katika nchi washirika.

Bidhaa ni kama mali zinazozalishwa viwandani mfano sabuni,dawa za

mswaki, matairi n.k., huduma ni kama tenda mbalimbali mfano tenda za

kutengeneza barabara, ugavi wa umeme,maji n.k. mitaji ni kama

uwekezaji katika sekta mbalimbali mfano kilimo,mabenki n.k. na pia

uanzishaji wa makazi na ukazi ni hatua ya mtu kutoka nchini mwake

kwenda kuishi kama raia mkazi katika nchi nyingine mshirika.


2. JE KUNA FAIDA GANI KWA TANZANIA KAMA NCHI KUINGIA KATIKA SOKO

HILI

Kwanza soko litaongeza ushindani katika biashara mfanO bidhaa za

viwandani jambo ambalo litawezesha kuzalishwa kwa bidhaa nyingi ,bora

na muhimu kwa watumiaji. Pia bidhaa hizo zitaweza kupatikana kwa

bei rahisi kutokana na ushindani mkubwa wa viwanda.


Pili soko litakuza ushirikiano imara ikiwa ni pamoja na kujenga

maelewano mema kati ya nchi washirika kupitia mwingiliano wa

wananchi na serikali zao na hivyo kuweka mazingira mazuri kisiasa na

kiuchumi katika ukanda wa Afrika Mashariki.


Tatu soko hili litaweka uwanja mpana na mrefu utakaoinua wepesi wa

kuuza na kununua bidhaa.mazao na mali nyingine tunazohitaji, mfano

kama mkulima alikuwa anategemea kuuza mazao yake katika masoko ya

Tanzania tu na mikoa yake sasa mkulima huyu atakuwa na uwezo wa

kuogelea katika masoko yote ya Afrika Mashariki kwa kadri anavotaka na

anavyoweza.


Nne soko litatoa uwanja mrefu na mpana wa ajira.Hii ni kwasababu

Mtanzania aliyekuwa na uwezo wa kutafuta ajira Tanzania na mikoa yake

pekee sasa ataweza kutafuta ajira Rwanda ,Burundi na kwingineko kwa

uhuru.


Tano soko litakuza viwango vya utafiti katuka nyanja ya teknolojia na

maendeleo ya jamii. Hili linatokana na ukweli kuwa jamii ya Afrika

Mashariki itakuwa imeunganisha nguvu katika kutekeleza malengo haya

badala ya kila nchi kuhangaika na mambo yake kama ilivyokuwa awali.


Sita soko la pamoja litawaweka pamoja raia wa Afrika Mashariki na

hivyo kuondoa ubaguzi uliokuwa unasababishwa na mataifa haya

kutengana. Mganda atakuwa kama Mkenya na Mkenya kama Mtanzania

n.k.Hili ni muhimu kutokana na undugu wa kihistoria uliopo katuika

ukanda huu.


Kwa uchache sana hizi ndizo baadhi ya faida za soko hili.


3. SOKO HILI LINAHIUSISHA MAENEO GANI YA MSINGI


i. HAKI NA MWINGILIANO HURU WA WATU KATIKA NCHI WASHIRIKA

Ibara ya 7(1) ya mkataba wa makubaliano wa soko la pamoja inasema

kuwa wananchi wa nchi washirika watakuwa huru na haki ya kutembea

katika nchi wanachama. Kutokana na hili Mtanzania atakuwa huru na haki

ya kwenda Rwanda, Mkenya atakuwa huru na haki ya kwenda Burundi n.k.


• JE KUNA KIBALI CHOCHOTE AU KITAMBULISHO UNACHOHITAJI KUWA NACHO

KATIKA UHURU WA KUTEMBEA KATIKA NCHI WANACHAMA?

Ndiyo kutakuwa na hati maaalum(pass) atakayotakiwa kuwa nayo mtu

anapokuwa katika mwingiliano wa nchi wanachama. Hati hii ( pass)

inatolewa bure na itakuwa inadumu kwa miezi sita tu. Baada ya miezi

sita mhusika atatakiwa kuisajili upya(renew). Hii ni tofauti na

wananchi wengi wanavyodhani kuwa hakuna hati au nyaraka yoyote

inayohitajika unapotembea katika nchi washirika. Kwa wanafunzi hati

hii itakuwa inasajiliwa upya(renew) kila mwaka na sio miezi sita kama

ilivyo kwa raia wengine.


Pia katika mwingiliano huu kunaweza kukawa na mipaka au masharti iwapo

kutatokea hali tete ya usalama au hatari za kiafya kama magonjwa ya

kuambukizwa n.k. Katika hali kama hii uhuru wa kutembeleana unaweza

kuwekewa masharti.


UHURU WA KUFANYA KAZI POPOTE KATIKA NCHI WANACHAMA

Ibara ya 10(1) inasema kuwa wafanyakazi katika nchi washirika

watakuwa huru kufanya kazi popote ndani ya nchi washirika. Katika

kulitekeleza hilo tarehe 1. 7. 2010 kila nchi ilieleza ni wafanyakazi

wa aina gani imewafungulia milango, Mfano Burundi inahitaji wataalam

wa aina zote, Kenya mameneja,mafundi, na wataalam wengine, Tanzania

mafundi na wataalam wengine,Rwanda mafundi na wataalam wengine, Uganda

mameneja na wataalam wengine.


JE MFANYAKAZI ATARUHUSIWA KUFANYA KAZI HATA KATIKA OFISI ZA

UMMA(PUBLIC SERVICE) KATIKA NCHI WASHIRIKA?

Hapana mfanyakazi hataruhusiwa kufanya Kazi katika ofisi au huduma za

umma, kwa mfano hataweza kutoka mfanyakazi Uganda akajakuwa

mkurugenzi wa TAKUKURU au gavana wa benki kuu,mbunge,mkuu wa mKoa

n.k. Anaweza kupata nafasi hizo iwapo tu sera na sheria za nchi husika

zinaruhusu kitu kama hicho.

UHURU NA HAKI YA KUWEKA MAKAZI POPOTE KATIKA NCHI WASHIRIKA

Ibara ya 14(1) inasema kuwa raia yeyote wa nchi washirika ana haki ya

kuweka makazi popote katika nchi washirika. Mfano Mtanzania anaweza

kutoka hapa na kwenda kuishi Burundi, Mganda akaishi Kenya n.k.


JE UNA UHURU WA KUWEKA MAKAZI POPOTE KATIKA NCHI WASHIRIKA BILA KIBALI

AU KITAMBULISHO CHOCHOTE.?

Hapana kutatakiwa kibali maalum(residence permit) kitakachokuwa

kinatolewa kwa ajili ya ukazi katika nchi washirika.Sio kweli kama

wananchi walio wengi wanavyojua kuwa raia atakuwa anaweza kuishi

popote bila kibali au hati yoyote ya kumtambulisha.


JE RAIA ATAKAPOKUWA POPOTE NDANI YA NCHI WASHIRIKA ATALINDWA NA SHERIA

ZA NCHI YAKE AU SHERIA ZA NCHI ALIPOHAMIA NA KUWEKA MAKAZI

Ibara ya 14(7) inasema kuwa suala lolote linalohusiana ukazi wa raia

katika nchi washirika litalindwa na sera za nchi husika yaani nchi

alikohamia mtu na kuweka makazi ikiwa ni pamoja na sheria za nchi

washirika.Kwa hiyo raia atapaswa kufuata sera za nchi alikohamia

kwanza na kwa upande mwingine atafuata sheria za jumuia.

Ibara ya14(2) inatoa haki kwa raia aliyepata ruhusa ya ukazi katika

nchi washirika kutumia hiyo haki hata kwa familia yake. Ina maana

haki ya ukazi ya baba inatumika hata kwa mtoto pamoja na mke wake.


UHURU NA HAKI YA KUPATA NA KUTUMIA ARDHI KATIKA NCHI WASHIRIKA

Ibara ya 15(1) inatoa haki kwa raia wa nchi washirika kununua na

kutumia ardhi katika nchi washirika. Ina maana Mtanzania ataweza

kumiliki ardhi Uganda, Burundi n.k. Vivyo hivyo Mganda au Mnyarwnda na

wengine wana haki ya kuimiliki ardhi Tanzania n.k. .


UHURU NA HAKI YA KUBADILISHANA HUDUMA KATIKA NCHI WASHIRIKA

Ibara ya 16(1) inatoa haki na uhuru wa raia pamoja na setrikali za

nchi wanachama kubadilishana huduma. Ubadilishanaji wa huduma upo kama

ifuatavyo:

Kwanza ugavi wa huduma kutoka nchi moja mshirika kwenda nchi nyingine

mshirika, mfano Uganda inaweza kugawa umeme Tanzania au Tanzania

inaweza kutoa ugavi wa maji Rwanda na mazingira mengine kama hayo.

Pili ugavi wa huduma wa nchi mshirika kuwahudumia wageni au watumiaji

wa huduma wanaofika katika nchi ile, mfano Tanzania kutoa huduma ya

utalii kwa wageni kutoka nchi washirika au Uganda kutoa huduma ya

elimu kwa wageni au watumia huduma hiyo wanaofika eneo lile n.k.

Tatu ni aina ya hudum zitakazokuwa zinatolewa na mashirika pamoja na

taasisi maalum za kihiduma katika nchi washirika. Mashirika na taasisi

hizi wanaweza kutoa huduma zozote kulingana na sera na sheria za nchi

husika.

Nne ni huduma zitakazokuwa zinatolewa na watu binafsi yaani raia

wenyewe wa nchi hizi popote katika nchi wanachama,mfano mtu binafsi wa

Tanzania atakuwa na uwezo labda wa kutoa huduma ya usafi katika

barabara fulani ndani ya nchi washirika, makampuni ya mawakili watatoa

huduma zao katika nchi wanachama,madaktari ,wahasibu na mainjinia nao

wataweza kutoa huduma popote katika nchi washirika.


Ibara ya 17 imazuia aina yoyote ya ubaguzi katika tenda za utoaji

huduma kwa kueleza kuwa kila nchi itapaswa kuiangalia nchi nyingine

kama inavyojiangalia yenyewe.


Pia nchi washirika zimekubaliana kuendelea kufungua sekta

ndogondogo kutoka katika sekta za biashara na taaluma,

mawasiliano,ugavi,elimu na fedha, utalii na huduma za safari na

usafirishaji.


UHURU NA HAKI YA KUWEKEZA MITAJI KATIKA NCHI WASHIRIKA

Mfano wa maana ya kuwekeza mitaji ni kama raia wa Kenya kununua

mashamba Tanzania,Rwanda au pengine, au raia katika nchi washirika

kujenga kiwanda au benki n.k

Ibara ya 24(1) inatoa haki hii ikiwa ni pamoja na sharti la kuondoa

vikwazo katila uwekezaji wa mitaji.

JE KWA SASA RAIA WA NCHI WASHIRIKA WANAWEZA KUWEKEZA MITAJI TANZANIA?

Hapana jambo hilo kwa saa haliwezekani. Kwa sasa jambo hilo

linawezekana Rwanda, Uganda na Kenya. Tanzania pamoja na Burundi

wameahidi kuruhusu uwekezaji wa mitaji katika kipindi hiki cha 2010

mpaka 2015.


JE USALAMA WA WATUMIA BIDHAA(RAIA) UMEZINGATIWA KUTOKANA NA USHINDANI

WA UZALISHAJI UTAKAOKUWEPO

Kwakuwa utakuwepo ushindani mkubwa katika uzalishaji hasa sekta ya

viwanda jumuia imeona ni muhimu kuweka uataratibu maaluma wa kulinda

usalama wa raia mtumia bidhaa. Ibara ya 36(1) inasema kuwa nchi

washirika zinapaswa kutanguliza mbele maslahi ya watumiaji wa bidhaa

ili kuwahakikishia afya na maisha bora na pia kuhakikisha ushindani wa

kibiashara inakuwa nyenzo ya raia kupata bidhaa kwa bei nafuu.

MATENDO YA KIBIASHARA YALIYOPIGWA MARUFUKU KATIKA SOKO LA PAMOJA

Ibara 33(1) inapiga marufuku tendo lolote linalolenga kuathiri uhuru

wa kibiashara

Ibaa ya 34(1) inapiga marufuku tendo lolote lialolenga kuzuia au

kuharibu ari ya ushindani katika soko.

Ibara vya 35 inazuia tendo lolote la ubaguzi katika ugavi wa huduma

pamoja na bidhaa katika nchi washirika

SEKTa NYINGINE MUHIMU ZILIZOLENGWA NA SOKO HILI

Kilimo na chakula, ushirika na maendeleo ya viwanda,uchumi na

muunagano katika sera za kifedha,usafirishaji na huduma nyingine za

kijamii,utafiti na maendeleo ya teknolojia, kulinda hakimiliki na na

ushirikiano wa kitakwimu na sekta nyinginezo.

No comments:

Post a Comment